skip to main
|
skip to sidebar
global
Pages
Home
Sunday, June 1, 2014
BALOZI WA UINGEREZA ALETA KASHESHE TANZANIA
Serikali imetangaza rasmi mgogoro wa kidiplomasia kati yake na Balozi wa Uingereza nchini ikimtaka kujieleza kwa madai ya kuingilia mambo ya ndani ya nchi.
Mgogoro huo ulitangazwa bungeni mjini Dodoma jana na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Steven Maselle aliyemtaka balozi huyo kufika Wizara ya Mambo ya Nje kujibu tuhuma hizo.
Kiini cha Serikali kumtuhumu balozi huyo ni hatua ya Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi) kuihusisha Uingereza na urejeshwaji wa Sh76 bilioni za chenji ya Rada.
“Katika mchango wake (Kafulila), ameongea jambo moja nyeti sana na hili bora niliseme ili liwe fundisho kwa wengine… Hii ni nchi huru baada ya mwaka 1961,” alisema Naibu Waziri
.
“Zimekuwapo ripoti kwamba Balozi wa Uingereza amekuwa akijihusisha kuratibu vikao mbalimbali katika Jiji la Dar es Salaam na Dodoma kinyume cha utaratibu na hadhi ya kidiplomasia.”
Huku akionyesha kuwa na hasira, Maselle aliongeza kusema: “Vikao hivyo vina malengo ya kuhujumu mipango na mikakati ya maendeleo, ushahidi huo upo na utakapohitajika utatolewa.”
“Inasikitisha na kuchukiza balozi wa taifa kama Uingereza akifanya vitendo kinyume cha maadili… Anahusishwa kushawishi marafiki wa maendeleo wasitishe misaada ya kibajeti kwa Tanzania,”alisema.
Balozi wa Uingereza
Hata hivyo, Mwananchi ilimtafuta Balozi wa Uingereza Dianna Melrose, azungumzie suala hilo, msemaji wake Tamsin Clayton ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Siasa, Miradi na Mahusiano alisema wameshtushwa na taarifa hizo, lakini kwa sasa hawawezi kusema chochote mpaka wafahamu chanzo cha tatizo.
Aidha Naibu waziri Maselle alisema kuwa hivi karibuni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), alikuja Tanzania na kwamba upo ushahidi kuwa Balozi huyo wa Uingereza, alitamka kuwa anafikiria kuishawishi Serikali yake isitoe fedha za Miradi ya Maendeleo ya Millenia (MCC2).
“Ni aibu kwa Serikali ya Waziri Mkuu, David Cameron kwa balozi wake kufanya uwakala wa Benki ya Standard Chartered, kuishawishi Serikali ya Tanzania ikope fedha ili kulipa kampuni binafsi,” alisema Maselle huku akipigiwa makofi na wabunge wengi wa CCM na kuongeza:
“Rais Kikwete amelikataa kwa nguvu zote…, Serikali haiwezi kubeba mzigo wa kampuni binafsi.”
Newer Post
Older Post
Home
Popular Posts
MUIGIZAJI AJIKATA UUME AKITAKA KUWA MWANAUME
Msanii Mrusi, Evgniv Sapaev, aliyecheza katika filamu mashuhuri ya ‘Burnt by the Sun 2′, alipoteza uume wake baada ya kuji...
BREAKING NEWS: MKE WA ALLY CHOKI AFARIKI DUNIA
MKURUGENZI wa bendi ya Extra Bongo, Ali Choki amepata pigo la kuondokewa na mke wake, Shuea Hamis ‘Mama Shuu’ baada ya kuugua kwa m...
Majibu ya Mbunge Salvatory Machemli kuhusu picha za utupu zilizosambazwa zenye sura yake.
Siku chache zilizopita kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii zilisambazwa picha mbalimbali za Wabunge wa Bunge la Tanzania zikiony...
MGOGORO:-MUFTI WA TANZANIA SHAABAN SIMBA AONGOZA BAADHI YA WAISLAM KUVUNJA MILANGO YA MSIKITI MKUU WA IJUMAA TABORA
Baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu msikiti mkuu wa Ijumaa Gongoni mjini Tabora wakati wa tukio la kuvunjwa milango ya msikiti...
WANAHARAKATI TANZANIA WAWALILI WASICHANA WALIOTEKWA NA BOKO HARAMU WAAMUA KUFANYA MAANDAMANO....
Wasichana wakiwa na mabango kudai kurudishwa kwa wasichana zaidi ya 200 waliotekwa na Boko Haram maandamano yakielekea viwa...
Jeshi la Polisi Latangaza kuanza Uchunguzi Wa Kina dhidi ya Freeman Mbowe , Dk. Slaa , Lissu, Mnyika na Godbless Lema Wanaotuhumiwa kwa Mauaji na Vitendo vya kigaidi
JESHI la Polisi limetangaza kuanzisha uchunguzi wa kina dhidi ya viongozi wa kitaifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...
Wanasheria wahoji uhalali wa Bunge la Katiba bila Ukawa
“Hakuna kifungu cha sheria kinachosema Rais anaweza kulivunja Bunge hilo, bali linaweza kuahirishwa. Nami ningeshauri lia...
NYOTA YA LOWASSA YAZIDI KUNG'AA BAADA YA KUZINDUA HELKOPTA YA KANISA LA GWAJIMA JIJINI DARESALAAM
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward...
BINTI WA MIAKA 16 YUPO HOI HOSPITALINI AKIUGUZA MAJERAHA KICHWANI BAADA YA KUNG'ATWA NA MWAJIRI WAKE
Vitendo vya unyanyasaji wa mabinti wa kazi majumbani vimeendelea kuripotiwa jijini Dar es Salaam baada ya binti mwingine Melina Mat...
KINANA : VIONGOZI WA KIJIJI WAACHE KUUZA ARDHI BILA KUWASHIRIKISHA WANANCHI
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na wamasai katika kijiji cha Ayamango (Gallapo) ambapo alikuwa na kazi ya kufu...
[URL=http://info.flagcounter.com/UhIW][IMG]http://s03.flagcounter.com/count/UhIW/bg_FFFFFF/txt_000000/border_CCCCCC/columns_2/maxflags_12/viewers_0/labels_0/pageviews_0/flags_0/[/IMG][/URL]
flags.es
www.playonlineroulettex.com
The following text will not be seen after you upload your website, please keep it in order to retain your counter functionality
silver lotto system review
Live Traffic Stats
Ads 468x60px
Followers
PGA Head Teaching Professional
Unknown
View my complete profile
Powered by
Blogger
.
BALOZI WA UINGEREZA ALETA KASHESHE TANZANIA
Serikali imetangaza rasmi mgogoro wa kidiplomasia kati yake na Balozi wa Uingereza nchini ikimtaka kujieleza kwa madai ya kuingilia mambo ya ndani ya nchi.
Mgogoro huo ulitangazwa bungeni mjini Dodoma jana na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Steven Maselle aliyemtaka balozi huyo kufika Wizara ya Mambo ya Nje kujibu tuhuma hizo.
Kiini cha Serikali kumtuhumu balozi huyo ni hatua ya Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi) kuihusisha Uingereza na urejeshwaji wa Sh76 bilioni za chenji ya Rada.
“Katika mchango wake (Kafulila), ameongea jambo moja nyeti sana na hili bora niliseme ili liwe fundisho kwa wengine… Hii ni nchi huru baada ya mwaka 1961,” alisema Naibu Waziri
.
“Zimekuwapo ripoti kwamba Balozi wa Uingereza amekuwa akijihusisha kuratibu vikao mbalimbali katika Jiji la Dar es Salaam na Dodoma kinyume cha utaratibu na hadhi ya kidiplomasia.”
Huku akionyesha kuwa na hasira, Maselle aliongeza kusema: “Vikao hivyo vina malengo ya kuhujumu mipango na mikakati ya maendeleo, ushahidi huo upo na utakapohitajika utatolewa.”
“Inasikitisha na kuchukiza balozi wa taifa kama Uingereza akifanya vitendo kinyume cha maadili… Anahusishwa kushawishi marafiki wa maendeleo wasitishe misaada ya kibajeti kwa Tanzania,”alisema.
Balozi wa Uingereza
Hata hivyo, Mwananchi ilimtafuta Balozi wa Uingereza Dianna Melrose, azungumzie suala hilo, msemaji wake Tamsin Clayton ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Siasa, Miradi na Mahusiano alisema wameshtushwa na taarifa hizo, lakini kwa sasa hawawezi kusema chochote mpaka wafahamu chanzo cha tatizo.
Aidha Naibu waziri Maselle alisema kuwa hivi karibuni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), alikuja Tanzania na kwamba upo ushahidi kuwa Balozi huyo wa Uingereza, alitamka kuwa anafikiria kuishawishi Serikali yake isitoe fedha za Miradi ya Maendeleo ya Millenia (MCC2).
“Ni aibu kwa Serikali ya Waziri Mkuu, David Cameron kwa balozi wake kufanya uwakala wa Benki ya Standard Chartered, kuishawishi Serikali ya Tanzania ikope fedha ili kulipa kampuni binafsi,” alisema Maselle huku akipigiwa makofi na wabunge wengi wa CCM na kuongeza:
“Rais Kikwete amelikataa kwa nguvu zote…, Serikali haiwezi kubeba mzigo wa kampuni binafsi.”
Newer Post
Older Post
Home