skip to main
|
skip to sidebar
global
Pages
Home
Sunday, June 1, 2014
BALOZI WA UINGEREZA ALETA KASHESHE TANZANIA
Serikali imetangaza rasmi mgogoro wa kidiplomasia kati yake na Balozi wa Uingereza nchini ikimtaka kujieleza kwa madai ya kuingilia mambo ya ndani ya nchi.
Mgogoro huo ulitangazwa bungeni mjini Dodoma jana na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Steven Maselle aliyemtaka balozi huyo kufika Wizara ya Mambo ya Nje kujibu tuhuma hizo.
Kiini cha Serikali kumtuhumu balozi huyo ni hatua ya Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi) kuihusisha Uingereza na urejeshwaji wa Sh76 bilioni za chenji ya Rada.
“Katika mchango wake (Kafulila), ameongea jambo moja nyeti sana na hili bora niliseme ili liwe fundisho kwa wengine… Hii ni nchi huru baada ya mwaka 1961,” alisema Naibu Waziri
.
“Zimekuwapo ripoti kwamba Balozi wa Uingereza amekuwa akijihusisha kuratibu vikao mbalimbali katika Jiji la Dar es Salaam na Dodoma kinyume cha utaratibu na hadhi ya kidiplomasia.”
Huku akionyesha kuwa na hasira, Maselle aliongeza kusema: “Vikao hivyo vina malengo ya kuhujumu mipango na mikakati ya maendeleo, ushahidi huo upo na utakapohitajika utatolewa.”
“Inasikitisha na kuchukiza balozi wa taifa kama Uingereza akifanya vitendo kinyume cha maadili… Anahusishwa kushawishi marafiki wa maendeleo wasitishe misaada ya kibajeti kwa Tanzania,”alisema.
Balozi wa Uingereza
Hata hivyo, Mwananchi ilimtafuta Balozi wa Uingereza Dianna Melrose, azungumzie suala hilo, msemaji wake Tamsin Clayton ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Siasa, Miradi na Mahusiano alisema wameshtushwa na taarifa hizo, lakini kwa sasa hawawezi kusema chochote mpaka wafahamu chanzo cha tatizo.
Aidha Naibu waziri Maselle alisema kuwa hivi karibuni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), alikuja Tanzania na kwamba upo ushahidi kuwa Balozi huyo wa Uingereza, alitamka kuwa anafikiria kuishawishi Serikali yake isitoe fedha za Miradi ya Maendeleo ya Millenia (MCC2).
“Ni aibu kwa Serikali ya Waziri Mkuu, David Cameron kwa balozi wake kufanya uwakala wa Benki ya Standard Chartered, kuishawishi Serikali ya Tanzania ikope fedha ili kulipa kampuni binafsi,” alisema Maselle huku akipigiwa makofi na wabunge wengi wa CCM na kuongeza:
“Rais Kikwete amelikataa kwa nguvu zote…, Serikali haiwezi kubeba mzigo wa kampuni binafsi.”
Newer Post
Older Post
Home
Popular Posts
BREAKING NEWS: MKE WA ALLY CHOKI AFARIKI DUNIA
MKURUGENZI wa bendi ya Extra Bongo, Ali Choki amepata pigo la kuondokewa na mke wake, Shuea Hamis ‘Mama Shuu’ baada ya kuugua kwa m...
Majibu ya Mbunge Salvatory Machemli kuhusu picha za utupu zilizosambazwa zenye sura yake.
Siku chache zilizopita kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii zilisambazwa picha mbalimbali za Wabunge wa Bunge la Tanzania zikiony...
MUIGIZAJI AJIKATA UUME AKITAKA KUWA MWANAUME
Msanii Mrusi, Evgniv Sapaev, aliyecheza katika filamu mashuhuri ya ‘Burnt by the Sun 2′, alipoteza uume wake baada ya kuji...
MGOGORO:-MUFTI WA TANZANIA SHAABAN SIMBA AONGOZA BAADHI YA WAISLAM KUVUNJA MILANGO YA MSIKITI MKUU WA IJUMAA TABORA
Baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu msikiti mkuu wa Ijumaa Gongoni mjini Tabora wakati wa tukio la kuvunjwa milango ya msikiti...
KINANA : VIONGOZI WA KIJIJI WAACHE KUUZA ARDHI BILA KUWASHIRIKISHA WANANCHI
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na wamasai katika kijiji cha Ayamango (Gallapo) ambapo alikuwa na kazi ya kufu...
MTOTO NASRA ALIYEISHI KATIKA BOKSI MIAKA MINNE SASA KUZIKWA LEO MAKABURI YA KOLLA BAADA YA WANANCHI KUAGA MWILI WAKE JAMHURI MANISPAA YA MOROGORO.
Jeneza lenye mwili wa mtoto Nasra Rashid (4) likishushwa kutoka kwenye gari ili kuingiza katika chumba cha kuhifadhia maiti hospitali...
HAIJAWAHI TOKEA..UKAWA WAWEKA HISTORIA IRINGA WAKUSANYA MAELFU YA WATU..Fungua hapa...
Profesa Ibrahim Lipumba akikaribishwa na Mchungaji Peter Msigwa (mbunge wa Iringa Mjini )kuhutubia mamia ya wakazi wa mji w...
CHADEMA YAIBUKA KIDEDEA KESI YAO MAHAKAMA YA NJOMBE DHIDI YA MBUNGE WA CCM
MAHAKAMA ya Wilaya ya Njombe imetupia mbali kesi iliyokuwa ikiwakabili viongozi wa CHADEMA mkoani hapa, ya kutishia kummwagia tindik...
WANAHARAKATI TANZANIA WAWALILI WASICHANA WALIOTEKWA NA BOKO HARAMU WAAMUA KUFANYA MAANDAMANO....
Wasichana wakiwa na mabango kudai kurudishwa kwa wasichana zaidi ya 200 waliotekwa na Boko Haram maandamano yakielekea viwa...
MCHUNGAJI ALIYEHARIBIWA SURA KWA TINDIKALI, SASA AENDELEA VYEMA
Mchungaji Umar Umulinde wa Uganda akiwa hospitalini. Hizi ni baadhi ya p...
[URL=http://info.flagcounter.com/UhIW][IMG]http://s03.flagcounter.com/count/UhIW/bg_FFFFFF/txt_000000/border_CCCCCC/columns_2/maxflags_12/viewers_0/labels_0/pageviews_0/flags_0/[/IMG][/URL]
flags.es
www.playonlineroulettex.com
The following text will not be seen after you upload your website, please keep it in order to retain your counter functionality
silver lotto system review
Live Traffic Stats
Ads 468x60px
Followers
PGA Head Teaching Professional
Unknown
View my complete profile
Powered by
Blogger
.
BALOZI WA UINGEREZA ALETA KASHESHE TANZANIA
Serikali imetangaza rasmi mgogoro wa kidiplomasia kati yake na Balozi wa Uingereza nchini ikimtaka kujieleza kwa madai ya kuingilia mambo ya ndani ya nchi.
Mgogoro huo ulitangazwa bungeni mjini Dodoma jana na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Steven Maselle aliyemtaka balozi huyo kufika Wizara ya Mambo ya Nje kujibu tuhuma hizo.
Kiini cha Serikali kumtuhumu balozi huyo ni hatua ya Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi) kuihusisha Uingereza na urejeshwaji wa Sh76 bilioni za chenji ya Rada.
“Katika mchango wake (Kafulila), ameongea jambo moja nyeti sana na hili bora niliseme ili liwe fundisho kwa wengine… Hii ni nchi huru baada ya mwaka 1961,” alisema Naibu Waziri
.
“Zimekuwapo ripoti kwamba Balozi wa Uingereza amekuwa akijihusisha kuratibu vikao mbalimbali katika Jiji la Dar es Salaam na Dodoma kinyume cha utaratibu na hadhi ya kidiplomasia.”
Huku akionyesha kuwa na hasira, Maselle aliongeza kusema: “Vikao hivyo vina malengo ya kuhujumu mipango na mikakati ya maendeleo, ushahidi huo upo na utakapohitajika utatolewa.”
“Inasikitisha na kuchukiza balozi wa taifa kama Uingereza akifanya vitendo kinyume cha maadili… Anahusishwa kushawishi marafiki wa maendeleo wasitishe misaada ya kibajeti kwa Tanzania,”alisema.
Balozi wa Uingereza
Hata hivyo, Mwananchi ilimtafuta Balozi wa Uingereza Dianna Melrose, azungumzie suala hilo, msemaji wake Tamsin Clayton ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Siasa, Miradi na Mahusiano alisema wameshtushwa na taarifa hizo, lakini kwa sasa hawawezi kusema chochote mpaka wafahamu chanzo cha tatizo.
Aidha Naibu waziri Maselle alisema kuwa hivi karibuni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), alikuja Tanzania na kwamba upo ushahidi kuwa Balozi huyo wa Uingereza, alitamka kuwa anafikiria kuishawishi Serikali yake isitoe fedha za Miradi ya Maendeleo ya Millenia (MCC2).
“Ni aibu kwa Serikali ya Waziri Mkuu, David Cameron kwa balozi wake kufanya uwakala wa Benki ya Standard Chartered, kuishawishi Serikali ya Tanzania ikope fedha ili kulipa kampuni binafsi,” alisema Maselle huku akipigiwa makofi na wabunge wengi wa CCM na kuongeza:
“Rais Kikwete amelikataa kwa nguvu zote…, Serikali haiwezi kubeba mzigo wa kampuni binafsi.”
Newer Post
Older Post
Home