skip to main
|
skip to sidebar
global
Pages
Home
Thursday, May 29, 2014
WATOTO WATATU WAFUNGIWA NDANI MWEZI MMOJA KWA HOFU YA KUBAKWA
Huyu ndiye mama aliyefungia watoto wake EVA MDEMU
Afisa Mtendaji wa kijiji cha Tanangozi Bi Lucy Msigwa akitupa taarifa ya kufungiwa kwa watoto hao.
Kushoto ni mwandishi wa habari wa Kwanza Jamii Mathias Canal, anayefuatia mwenye shati jekundu ni mtuhumiwa wa ubakaji na kulawiti Juma Msungu, kulia ni mwandishi wa Nuru Fm Victor Meena, tukipata maelezo juu ya tuhuma alizonazo kijana huyo.
katikati ni Rajabu Michael Kigwamke baba wa mtoto
aliyelawitiwa akiwa na umri wa miaka 4
,
kushoto ni Mathias Canal mwandishi wa Kwanza Jamii, kulia ni Victor Meena Mwandishi wa Nuru Fm, akitupa maelezo juu ya kumchukua mtoto wake baada kupata taarifa ya kufungiwa ndani kwa muda mrefu.
Na Mathias Canal
Tukio hilo limetokea hivi karibuni katika kijiji cha Tanangozi kata ya Mseke Wilaya ya Iringa Vijijini, Mkoani Iringa ambapo mama aliyefahamika kwa jina la Eva Mdemu anayefanya biashara ndogo ndogo kijijini hapo alikutwa akiwa amewafungia watoto hao ndani ya nyumba yake kwa takribani mwezi mmoja.
Mama huyo amesema kuwa sababu iliyopelekea kuwafungia watoto hao katika chumba kichafu ambacho hutumika pia kwa haja kubwa na ndogo kwa watoto hao, ni kutokana na hofu ya kubakwa kwa watoto hao, ambao takribani miezi saba iliyopita mtoto wake wa kike mwenye umri wa miaka 10 alibakwa, na mtoto wake wa kiume mwenye umri wa miaka 4 alilawitiwa na kijana aliyefahamika kwa jina la Juma Msungu mkazi wa Tanangozi mwenye umri wa miaka 20.
Eva amekiri kuwafungia watoto hao na kuwapa chakula dirishani, hata hivyo amesema kuwa yeye ni mama wa watoto sita ambao baba zao wote hawatoi huduma kwa watoto hao, na huwafungia pale anapoondoka kwa ajili ya kwenda kwenye biashara yake ambayo ndiyo inayomuwezesha kuwahudumia watoto hao.
Hata hivyo Eva amesema kuwa baadhi ya wanakijiji wamekuwa wakimtishia kumhamisha katika kijiji hicho huku Rajabu Michael Kigwamke ambaye ni baba wa mtoto aliyelawitiwa amemchukua mtoto huyo kwa lazima kutokana na kuogopa kupatwa na magonjwa mbalimbali yanayoshabihana na uchafu, wakati hajawahi kumhudumia mtoto huyo tangu alipomzaa miaka sita iliyopita.
Sambamba na hayo mama huyo ameiomba serikali kumsaidia kutokana na adha kubwa aliyonayo ya kubakwa kwa watoto wake huku mtuhumiwa wa kesi hiyo ya ubakaji akiwa ameachiwa huru baada ya kuwa kizuizini takribani miezi sita tu.
Kwa upande wao wananchi waliojitokeza kwenye adha hiyo ambayo ilihudhuriwa na viongozi wa kijiji, wamekiri kufungiwa ndani kwa watoto hao ambao walikuwa kwenye chumba chenye uchafu uliokithiri.
Sambamba na hayo wanakijiji hao wamesema kuwa mama huyo anajihusisha na mambo ya kishirikina, kwani ameanza muda mrefu kuwafungia watoto hao japo wakati Juma akiwa ameshikiliwa na jeshi la polisi watoto hao waliendelea kubakwa ndani kwao huku milango yote ikiwa imefungwa na kufuli.
Rajabu Michael Kigwamke ambaye ni baba wa mtoto huyo aliyewahi kubakwa alikanusha kutomhudumia mtoto huyo na kudai kuwa amekuwa akishirikiana na mke wake huyo katika baadhi ya huduma ikiwa ni elimu pamoja na mavazi.
Kigwamke amesema kuwa baada ya kupata taarifa ya kubakwa na kulawitiwa kwa watoto hao aliamua kumkamata Juma Msungu mtuhumiwa wa tukio hilo ila ajabu ni pale ambapo mtuhumiwa huyo alikuwa kizuizini, lakini bado watoto hao waliendelea kubakwa.
Juma Msungu ni kijana mwenye umri wa miaka 20 yeye amekanusha kubaka na kulawiti watoto hao, huku akiongeza kuwa ameachiwa huru kutokana na mama huyo kushindwa kufika katika mahakama ya Wilaya.
Msungu aliongeza kuwa kama kweli yeye alikuwa ni mbakaji kwanini wakati watoto hao wanaenda hospitalini kupimwa yeye hakuchukuliwa vipimo vyovyote badala yake alipelekwa moja kwa moja kituo cha polisi.
Aidha akitoa taarifa hiyo Afisa Mtendaji wa kijiji cha Tanangozi Bi Lucy Msigwa alisema kuwa tarehe 26 mwezi huu wa tano alipigiwa simu na mgambo wa kijiji Bw Rajabu Michael Kigwamke kwamba kuna watoto wamefungiwa ndani ya nyumba yake na baada ya kufika katika eneo la tukio aliwakuta watoto hao wakiwa wamefungiwa ndani huku wakiwa uchi wa mnyama, watoto hao walikuwa watatu, wawili ni mapacha wana umri wa miaka 2 na Yule ambaye ni mkubwa ana miaka 5.Afisa mtendaji alimuamuru balozi kuufungua ule mlango na kuwachukua watoto hao kwenda nao hadi ofisi za serikali ya kijiji hadi pale alipofika mama huyo na kukiri kuwafungia watoto hao kutokana na kuogopa watoto wake kuendelea kubakwa hivyo aliamua kumkabidhi mtoto mmoja wa kiume kwa baba yake.
Newer Post
Older Post
Home
Popular Posts
MUIGIZAJI AJIKATA UUME AKITAKA KUWA MWANAUME
Msanii Mrusi, Evgniv Sapaev, aliyecheza katika filamu mashuhuri ya ‘Burnt by the Sun 2′, alipoteza uume wake baada ya kuji...
BREAKING NEWS: MKE WA ALLY CHOKI AFARIKI DUNIA
MKURUGENZI wa bendi ya Extra Bongo, Ali Choki amepata pigo la kuondokewa na mke wake, Shuea Hamis ‘Mama Shuu’ baada ya kuugua kwa m...
MGOGORO:-MUFTI WA TANZANIA SHAABAN SIMBA AONGOZA BAADHI YA WAISLAM KUVUNJA MILANGO YA MSIKITI MKUU WA IJUMAA TABORA
Baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu msikiti mkuu wa Ijumaa Gongoni mjini Tabora wakati wa tukio la kuvunjwa milango ya msikiti...
Majibu ya Mbunge Salvatory Machemli kuhusu picha za utupu zilizosambazwa zenye sura yake.
Siku chache zilizopita kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii zilisambazwa picha mbalimbali za Wabunge wa Bunge la Tanzania zikiony...
WANAHARAKATI TANZANIA WAWALILI WASICHANA WALIOTEKWA NA BOKO HARAMU WAAMUA KUFANYA MAANDAMANO....
Wasichana wakiwa na mabango kudai kurudishwa kwa wasichana zaidi ya 200 waliotekwa na Boko Haram maandamano yakielekea viwa...
Jeshi la Polisi Latangaza kuanza Uchunguzi Wa Kina dhidi ya Freeman Mbowe , Dk. Slaa , Lissu, Mnyika na Godbless Lema Wanaotuhumiwa kwa Mauaji na Vitendo vya kigaidi
JESHI la Polisi limetangaza kuanzisha uchunguzi wa kina dhidi ya viongozi wa kitaifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...
Wanasheria wahoji uhalali wa Bunge la Katiba bila Ukawa
“Hakuna kifungu cha sheria kinachosema Rais anaweza kulivunja Bunge hilo, bali linaweza kuahirishwa. Nami ningeshauri lia...
NYOTA YA LOWASSA YAZIDI KUNG'AA BAADA YA KUZINDUA HELKOPTA YA KANISA LA GWAJIMA JIJINI DARESALAAM
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward...
BINTI WA MIAKA 16 YUPO HOI HOSPITALINI AKIUGUZA MAJERAHA KICHWANI BAADA YA KUNG'ATWA NA MWAJIRI WAKE
Vitendo vya unyanyasaji wa mabinti wa kazi majumbani vimeendelea kuripotiwa jijini Dar es Salaam baada ya binti mwingine Melina Mat...
KINANA : VIONGOZI WA KIJIJI WAACHE KUUZA ARDHI BILA KUWASHIRIKISHA WANANCHI
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na wamasai katika kijiji cha Ayamango (Gallapo) ambapo alikuwa na kazi ya kufu...
[URL=http://info.flagcounter.com/UhIW][IMG]http://s03.flagcounter.com/count/UhIW/bg_FFFFFF/txt_000000/border_CCCCCC/columns_2/maxflags_12/viewers_0/labels_0/pageviews_0/flags_0/[/IMG][/URL]
flags.es
www.playonlineroulettex.com
The following text will not be seen after you upload your website, please keep it in order to retain your counter functionality
silver lotto system review
Live Traffic Stats
Ads 468x60px
Followers
PGA Head Teaching Professional
Unknown
View my complete profile
Powered by
Blogger
.
WATOTO WATATU WAFUNGIWA NDANI MWEZI MMOJA KWA HOFU YA KUBAKWA
Huyu ndiye mama aliyefungia watoto wake EVA MDEMU
Afisa Mtendaji wa kijiji cha Tanangozi Bi Lucy Msigwa akitupa taarifa ya kufungiwa kwa watoto hao.
Kushoto ni mwandishi wa habari wa Kwanza Jamii Mathias Canal, anayefuatia mwenye shati jekundu ni mtuhumiwa wa ubakaji na kulawiti Juma Msungu, kulia ni mwandishi wa Nuru Fm Victor Meena, tukipata maelezo juu ya tuhuma alizonazo kijana huyo.
katikati ni Rajabu Michael Kigwamke baba wa mtoto
aliyelawitiwa akiwa na umri wa miaka 4
,
kushoto ni Mathias Canal mwandishi wa Kwanza Jamii, kulia ni Victor Meena Mwandishi wa Nuru Fm, akitupa maelezo juu ya kumchukua mtoto wake baada kupata taarifa ya kufungiwa ndani kwa muda mrefu.
Na Mathias Canal
Tukio hilo limetokea hivi karibuni katika kijiji cha Tanangozi kata ya Mseke Wilaya ya Iringa Vijijini, Mkoani Iringa ambapo mama aliyefahamika kwa jina la Eva Mdemu anayefanya biashara ndogo ndogo kijijini hapo alikutwa akiwa amewafungia watoto hao ndani ya nyumba yake kwa takribani mwezi mmoja.
Mama huyo amesema kuwa sababu iliyopelekea kuwafungia watoto hao katika chumba kichafu ambacho hutumika pia kwa haja kubwa na ndogo kwa watoto hao, ni kutokana na hofu ya kubakwa kwa watoto hao, ambao takribani miezi saba iliyopita mtoto wake wa kike mwenye umri wa miaka 10 alibakwa, na mtoto wake wa kiume mwenye umri wa miaka 4 alilawitiwa na kijana aliyefahamika kwa jina la Juma Msungu mkazi wa Tanangozi mwenye umri wa miaka 20.
Eva amekiri kuwafungia watoto hao na kuwapa chakula dirishani, hata hivyo amesema kuwa yeye ni mama wa watoto sita ambao baba zao wote hawatoi huduma kwa watoto hao, na huwafungia pale anapoondoka kwa ajili ya kwenda kwenye biashara yake ambayo ndiyo inayomuwezesha kuwahudumia watoto hao.
Hata hivyo Eva amesema kuwa baadhi ya wanakijiji wamekuwa wakimtishia kumhamisha katika kijiji hicho huku Rajabu Michael Kigwamke ambaye ni baba wa mtoto aliyelawitiwa amemchukua mtoto huyo kwa lazima kutokana na kuogopa kupatwa na magonjwa mbalimbali yanayoshabihana na uchafu, wakati hajawahi kumhudumia mtoto huyo tangu alipomzaa miaka sita iliyopita.
Sambamba na hayo mama huyo ameiomba serikali kumsaidia kutokana na adha kubwa aliyonayo ya kubakwa kwa watoto wake huku mtuhumiwa wa kesi hiyo ya ubakaji akiwa ameachiwa huru baada ya kuwa kizuizini takribani miezi sita tu.
Kwa upande wao wananchi waliojitokeza kwenye adha hiyo ambayo ilihudhuriwa na viongozi wa kijiji, wamekiri kufungiwa ndani kwa watoto hao ambao walikuwa kwenye chumba chenye uchafu uliokithiri.
Sambamba na hayo wanakijiji hao wamesema kuwa mama huyo anajihusisha na mambo ya kishirikina, kwani ameanza muda mrefu kuwafungia watoto hao japo wakati Juma akiwa ameshikiliwa na jeshi la polisi watoto hao waliendelea kubakwa ndani kwao huku milango yote ikiwa imefungwa na kufuli.
Rajabu Michael Kigwamke ambaye ni baba wa mtoto huyo aliyewahi kubakwa alikanusha kutomhudumia mtoto huyo na kudai kuwa amekuwa akishirikiana na mke wake huyo katika baadhi ya huduma ikiwa ni elimu pamoja na mavazi.
Kigwamke amesema kuwa baada ya kupata taarifa ya kubakwa na kulawitiwa kwa watoto hao aliamua kumkamata Juma Msungu mtuhumiwa wa tukio hilo ila ajabu ni pale ambapo mtuhumiwa huyo alikuwa kizuizini, lakini bado watoto hao waliendelea kubakwa.
Juma Msungu ni kijana mwenye umri wa miaka 20 yeye amekanusha kubaka na kulawiti watoto hao, huku akiongeza kuwa ameachiwa huru kutokana na mama huyo kushindwa kufika katika mahakama ya Wilaya.
Msungu aliongeza kuwa kama kweli yeye alikuwa ni mbakaji kwanini wakati watoto hao wanaenda hospitalini kupimwa yeye hakuchukuliwa vipimo vyovyote badala yake alipelekwa moja kwa moja kituo cha polisi.
Aidha akitoa taarifa hiyo Afisa Mtendaji wa kijiji cha Tanangozi Bi Lucy Msigwa alisema kuwa tarehe 26 mwezi huu wa tano alipigiwa simu na mgambo wa kijiji Bw Rajabu Michael Kigwamke kwamba kuna watoto wamefungiwa ndani ya nyumba yake na baada ya kufika katika eneo la tukio aliwakuta watoto hao wakiwa wamefungiwa ndani huku wakiwa uchi wa mnyama, watoto hao walikuwa watatu, wawili ni mapacha wana umri wa miaka 2 na Yule ambaye ni mkubwa ana miaka 5.Afisa mtendaji alimuamuru balozi kuufungua ule mlango na kuwachukua watoto hao kwenda nao hadi ofisi za serikali ya kijiji hadi pale alipofika mama huyo na kukiri kuwafungia watoto hao kutokana na kuogopa watoto wake kuendelea kubakwa hivyo aliamua kumkabidhi mtoto mmoja wa kiume kwa baba yake.
Newer Post
Older Post
Home